NJIA ZA KUJIKWAMUA KATIKA MAISHA YA DHIKI

By MZ TECHNOLOGY
Fri, 21-Oct-2022, 13:34

Watu wengi wanashindwa kujua maana halisi ya mtaji.

Wengi wanafikiri labda mtaji lazima iwe fedha, lakini kiukweli mtaji ni

zaidi ya fedha. mtaji inaweza kuwa ni vingi vingi mbali na fedha.

Mtaji ni nini?

Mtaji ni kitu chochote ambacho unaweza kutumia kuanzishia biashara

yako na kupata faida. kwa hiyo mara nyingine sio fedha inaweza kuwa ni

kitu fulani cha aina fulani, linaweza kuwa ni jambo fulani, mahusiano ,ni

watu, ni mtandao ulionao, labda ni wazo zuri sana unakuwa nalo, ama ni

jina jema katika jamii.

Kwa hiyo vyote hivi vinaweza kuwa ni mtaji wa kuanza na kudumu

ambavyo vinaweza kubadilishwa na kuwa katika form ya pesa.

Kumbe mtaji sio fedha tu.

Njia hizo ni kama ifuatavyo

1. Mtaji mbadala

Tunapozungumzia mtaji mbadala hapa tunamaanisha ni yale mambo

ambayo ingebidi utumie fedha hutatumia fedha , utatumia kwa mfano

nguvu zako mwenyewe, au jasho mwenyewe,, au maarifa fulani,au jina

mtu mwingine, au utakopa ,au kuazima , au ubunifu, ndio unakuwa tayari

umetumia mtaji mbadala. kwa mfano kipaji ulichonacho au uzoefu fulani

au uwezo binafsi uliojijengea n.k

A. Kipaji Ulichonacho:

Mfano Masanja leo hii ni maarufu sana kwa sababu ametumia kipaji

chake cha kuchekesha kuwa mjasiriamali mzuri, Hakuhitaji pesa kufanya

ujasiriamal wake.

B. Uzoefu ulionao

Hili watu hawajui kama ni mtaji mbadala utakuta wanasema '' AAah

mimi ni mwalimu tu wa chekechea'' nifanye biashara gani, akasema sina

mtaji'' nikamwambia " huna sebule? akasema 'ninayo ' nikamwambia

anzia hapo hapo, na kufikia leo hii dada Hadija ana shule 3 za

chekechea Dar es salaam

C. Maarifa uliyonayo ambayo wengine hawana

Tunaposema maarifa mbalimbali mfano leo hii watu wananilipa kwa

kusikiliza kwa sababu nina maarifa ya kutatua matatizo ya watu

waliyonayo kijasiriamali.

D. Elimu yako

Mfano una cherehani iko ndani, kwa nini usianze kushona? wamiliki

wengi wa makampuni makubwa ya ushonaji walianza hivyo hivyo

2. Kupata mtaji kwa ndugu, jamaa na marafiki

Watu wengi wanakuwa kwenye umaskini wakati wamezungukwa na

ndugu matajiri kisa wanaona aibu kuomba msaada, lakini amini usiamini

watu wengi wametajirika kupitia ndugu, jamaa na marafiki,

Mfano mtu tajiri kuliko wote barani Afrika kutoka Nigeria ndugu Dangote

yeye alivyotaka kuanza ujasiriamali aliomba msaada toka kwa mjomba

wake ambaye alimuazima kama milioni 3 hivi kwa kuwa aliona fursa

kwenye mambo ya ujenzi (cement).

Dangote akaanza kununua cement na kuuza leo hii ndugu Dangote

amekuwa bilionea ambaye amewekeza sana barani Afrika anauza

cement, unga , mchele, mafuta, sukari na saa hivi anauza mafuta kule

Africa Magharibi hata hapa Tanzania tuna kiwanda chake kule Mtwara,

Kuomba msaada sio ishara ua udhaifu bali ni ishara ya nguvu kwamba

unajiamini ndio maana unaomba msaada. kumbuka kwenye neno

UJASIRIAMALI kuna neno Jasiri pia, huwezi kuwa na mali bila kuwa

jasiri.Umezungukwa na watu waliobarikiwa usisite kuwaambia

wakusaidie ,.

3. Kujiwekea akiba

Watu wengi sana hapa kwetu Tanzania ukiwaambia weka akiba

wanakwambia mimi siwezi kuweka akiba, sina utamaduni wa kuweka

akiba,

Hivyo mi nakushauri anza leo kujifunza kuweka akiba, ni ngumu sana

kufika juu bila kuweka akiba kwa mfano kama umeajiriwa na unajua

biashara fulani inataka milioni 2 ili kuifanya na wewe mshahara wako ni

laki 4,

Kwa nini basi kila mwezi usiweke laki 1 pembeni, ndani ya miaka miwili

utakuwa na milioni 2.4 huo ni mtaji wako wewe mwenyewe.

Usisite kuanza kidogo kwa kuweka akiba polepole mpaka ufike huko

unakoenda

4. Pata Mtaji kwa njia ya kudunduliza

Hii njia ya kudunduliza ndio njia ambayo ni nyepesi kabisa ambayo watu

wengi hawaioni, ukiamua kutumia njia hii kamwe huwezi kukosa mtaji,

Hii ina maana unaanza katika hali ya chini kabisa ya kufanya kitu

chochote halafu ile faida unayoipata hauitumii bali unaiwekeza kwenye

biashara yako.


Zingatia semina niliyo kupatia anzisha biashara leo njoo inbox nikupe fursa itakayo kusaidia kuwa milionea kwa mtaji wa laki mbili Tsh:200,000.

Tags:

#post

Related Habari

This site was designed with Websites.co.in - Website Builder

WhatsApp Google Map

Safety and Abuse Reporting

Thanks for being awesome!

We appreciate you contacting us. Our support will get back in touch with you soon!

Have a great day!

Are you sure you want to report abuse against this website?

Please note that your query will be processed only if we find it relevant. Rest all requests will be ignored. If you need help with the website, please login to your dashboard and connect to support

;